Sunday 24 April 2016

R.I.P PAPA WEMBA

Papa Wemba a Congolese Music star dies after stage collapse,he is one of   influential music figure in Congo has died aged 66 during a live concert in Ivory Cost.Papa Wemba a star for more than  four decades has met his demise while he was on duty.These are some of the hit song:Show me the Way  

The photo above was taken during one of Papa Wemba performance in Paris,
Africa has lost one of the greatest talent ever had



Saturday 15 November 2014

"MTOTO WA MIAKA 5 AFAULU MTIHANI WA MICROSOFT"


Mtoto huyo anaetokea Coventry amekua ndiye mtu mwenye umri mdogo sana kuwa na ujuzi wa maswala ya Computer duniani.Mtoto huyo anaekwenda kwa jina la Ayan Qureshi sasa ni Microsoft Certified Proffessional (MCP) baada ya kufaulu mtihani wa kiufundi unaotungwa na na kuratibiwa na Microsoft akiwa na umri wa miaka mitano (5) tu.

        Ayan ambae kwa sasa ana miaka 6,baba yake ni mtaalamu na mshauri kwenye maswala ya teknolojia,ametengeneza mtandao wa komputa nyumbani.





Wednesday 29 October 2014

"KUTANA NA KIJANA ANAYETENGENEZA MAMILIONI YA PESA KWA KUSAFISHA VIATU"






















Haijalishi ni aina gani ya viatu gani unavaa katika mkutano muhimu wa biashara swala kubwa la msingi ni viwe vinang'aa na vyenye mvuto.Picha juu hapo inaonesha kijana aliyekuwa maarufu kwa uuzaji wa Mayai akifanya kazi yake ya 'Shoe Shiner'.Kijana huyo anaekwenda kwa jina la Lere Mgayiya anasema wana kampuni kubwa ya kusafisha viatu kwa Afrika nzima,"Wakiwa ndani ya Johansburg wanasafisha pea 350 kwa siku ,Pea 120 Capetown,na 120 zingine kutoka Durban.Kampuni yake imeajiri wafanyakazi 45 ambao kwa sasa wametawanyika kwenye Viwanja vya ndege vitatu.Hadi sasa ana utajiri wa Randi Milioni 2.5 sawa na Dola 227,000 kwa kazi hiyo....

Thursday 16 October 2014

"USHAWAHI KUONA MASHINDANO YA NDEVU?",ANGALIA WATU NA NDEVU ZAO NI SHEEEEDA...!!






















   Dunia ina mambo na vijambo,ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni,duniani watu tumezoea kuona mashabiki wa fani mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu,gofu,nk.Ila mwaka huu 25/10/2014 kutakuwa na shindano maarufu la "NDEVU NA MUSTACHI",litakalofanyika Portland,Oregon.Inatarajiwa watu 3000 ''Wenye Ndevu''  kuhudhuria shindano hilo na watashindana  katika vipengele mbalimbali....!!!



Tuesday 14 October 2014

"KAMA KUBUSU TU UNAFUKUZWA KAZI,JE UKILA RUSHWAAA ITAKUAJE''

ASKARI WAKIWA WANAPEANA MABUSU MOTO MOTO MUDA WA KAZI.

Ni muda upi ambao ni muafaka kwa wewe kumbusu rafiki au mtu wako wa karibu?,Picha hapo juu inaonesha askari wawili wakipigana busu lililopelekea wao kupoteza kazi ''KWA AJILI YA BUSU TU?''.Kwa mtazamo wa kawaida hawa askari wawili hawakufikiria kama swala lingefika hatua mbaya ya kupelekea kufukuzwa kazi.Picha hiyo iliyopigwa Kagera-Kaskazini Magharibi mwa Tanzania-Ikionesha wawili hao wakipeana busu huku wakiwa wamevalia unifomu za kazini na hicho tu kilichukuliwa kama kigezo cha kuwafukuza kazi.

Picha hiyo iliyopakiwa kwenye intanenti na askari wa tatu,ambaye ndiye aliyepiga picha hiyo,iliyoibua mamlaka husika kulivalia njuga swala hilo,ndani ya Mamlaka ya Polisi mjini Kagera.Henry Mwaibambe ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa akiongea na BBC kuhusu hatua zilizochukuliwa,na kutetea maamuzi ya idara.Ingawa kwenye mitandao mingi ya kijamii watu wengi wamekua na maoni tofauti" niliwahi kuona picha ya aliyekua Raisi wa Marekani Reagan akimbusu mke wake,na hakuna aliyetaka kumwajibisha'',Mwingine akaongezea kwa kusema "Akari wawili wanapobusiana adhabu yao ni kubwa kuliko wala rushwa"
















Sunday 12 October 2014

"KIMBUNGA HUD HUD CHALETA MAAFA NCHINI INDIA''

  Kimbunga cha Hud Hud kinaendelea kimeuvuruga ukanda wa mashariki wa India,na kusababisha uharibifu uliopelekea kuwaondoa watu 350,000 kama hatua za usalama kwa raia hao.

   Hata hivyo inasemekana watu watatu wamekufa katika mji Andhra Pradesh na watatu pia katika mji wa Orissa.Kimbunga hicho kilichowekwa kwenye kundi ''Madhara sana'' kimeleta upepo uliokuwa unasafiri kwa mwendo kasi wa kilometa 205 kwa saa (205Km/h),kilivyokua kinapita pwani ya karibu na jiji la Visakhapatnam.Upepo huo mkali na mvua zimesababisha uharibifu wa miti,kukatika kwa huduma ya umeme pia uharibifu wa mazao shambani na majengo katika miji yote miwili.


KWA HABARI ZAIDI>>>